Na Mwandishi Wetu, Timesmajira Online
KLABU ya Simba imefikia makubaliano ya pande zote mbili ya kuvunja mkataba na Kocha Mkuu wa kikosi cha kwanza Roberto Oliveira Goncalves Do Carmo (Robetinho), sambamba na kocha wa viungo Corneille Hategekimana.
Kwa mujibu wa taarifa kutoka Simba SC leo, kupitia kwenye mitandao yake ya kijamii, klabu hiyo inawashukuru Makocha hao kwa mchango wao ndani ya klabu hiyo na kuwatakia kila la heri katika majukumu yao mapya.
Aidha, Simba SC imethibitisha kuwa kikosi hicho kitakuwa chini ya Kocha Daniel Cadena akisaidiwa na Seleman Matola katika kipindi hichi cha mpito huku mchakato wa kutafuta makocha wapya ukitarajiwa kukamilika hivi karibuni.

More Stories
Kasulu FC mabingwa mashindano Khimji 2025
Fainali Khimji cup kufanyika Februari 7,2025
Naibu Waziri wa Fedha abariki ujio mpya wa Bahati Nasibu