May 14, 2024

Timesmajira

Gazeti Huru La Kila Siku

Kada wa CCM ajitosa Udiwani Kipawa

Na David John, timesmajira, online

KADA wa Chama Cha Mapinduzi CCM, Kata ya kipawa wilayani ilala mkoani Dar es Salaam Mabindo Ngulu amechukuwa fomu ya udiwani wa kata hiyo baada ya kujipima na kuona anauwezo wa kuwaongoza wanakipawa.

Ngulu amesema kuwa kata ya kipawa imekuwa mikononi mwa upinzani na kusababisha kudorola kwa Maendeleo hivyo kutokana na hali hiyo ameshawishika kuchukua fomu ili kuweza kuwania nafasi ya kuwa Diwani wa Kata hiyo.

Akizungumza na Times Majira leo baada ya kuchukuwa fomu amesema kuwa amesukumwa kufanya hivyo kutokana na kata hiyo kukosa kiongozi sahihi ngazi ya kata na kuweza kuwatumikia wananchi wa kata ya kipawa.

Katibu Kata tawi la CCM Kipawa, Hassani Mwambanda (kulia), akimkabidhi fomu ya kuomba kuwania udiwani, Mabindo Ngulu. Mabindo amechukua fomu hiyo leo ambapo makabidhiano hayo yalifanyika Jijini Dar es Salaam. Picha na Prona Mumwi

“Leo kama mnavyoona ndungu zangu wanahabari nimejitosa kuchukua fomu hii kwa nia moja tu ya kupata ridhaa ya kuwatumikia wananchi wa kata yangu ya kipawa.”amesema na kuongeza

“Sasa hivi ni muda wa kuchukua fomu tu na kwenda kuijaza na baadae narudisha, michakato ndani ya chama itakapokamilika na hatimaye jina langu kurudi hapo sasa nitasema mipango yangu zaidi ,”amesema

Akizungumzia uzoefu wake kwenye siasa amesema yupo kwenye siasa kwa miaka mingi na Kama ilivyoada kwa wanasiasa hata yeye ameshapita vyama vingine huko nyuma lakini sasa yuko ndani ya Chama Cha Mapinduzi CCM na alishawahi kugombea nafasi kadhaa.

Pia amesema kutoka na utaalamu wake wa kuchanganua vitu anaamini anauwezo mkubwa wa kufanya jambo endapo Chama chake kitampa ridhaa na kupitishwa kuwa mgombea udiwani kwenye kata hiyo