Na Esther Macha, Timesmajira Online,Songwe
JAMII imetakiwa kulinda na kutunza miradi inayowekezwa na wawekezaji wazawa katika maeneo mbalimbali nchini ili iweze kuwanufaisha wananchi na kuwainua kiuchumi.
Akizungumza na waandishi wa habari waliotembelea Kijiji cha Masangula ,Diwani wa Kata ya Nyimbili Jimbo la Vwawa mkoa wa Songwe Tinson Nzunda ambaye ni Mwekezaji wa kampuni ya Lima amesema uwepo wa wawekezaji katika maeneo mbalimbali umekuwa na manufaa kwa wananchi .

Ameeleza kuwa wananchi wengi waliopo katika kijiji hicho maisha yao yanategemea ajira za muda mfupi kupitia uwekezaji aliofanya na kwamba hakuna mwananchi ambaye ataharibu miradi hiyo.
“Tunaomba serikali iendeleee kutuwekea mazingira rafiki wawekezaji ili tuendelee kufanya kazi kwa uhuru,”amesema.
Bonifasi Kibona ni mkazi Tunduma mkoani Songwe ambaye ni dereva katika kampuni hiyo huku kazi yake ni kupeleka miche ya kahawa kwenye mashamba na kazi zingine zinahusu shughuli za shamba.

Kibona amesema kupitia Mwekezaji huyo maisha yake yamebadilika kwani ameweza kusomesha watoto wake pamoja na kuendeleza kilimo nyumbani kwake pamoja na ufugaji wa mifugo mbalimbali .

More Stories
Yas yazidi kuboresha huduma sekta ya Utalii
ZOLA yajipanga kupeleka Nishati Safi kwa Watanzania, yaunga Mkono Juhudi za Rais Samia
Kiongozi wa Mwenge awataka RUWASA kukamilisha mradi wa maji kwa wakati Kilindi