Na Heri Shaaban, Timesmajira Online-Dar-es-Salaam
HALMASHAURI ya Jiji la Dar-es-Salaam kipitia Idara ya Elimu Msingi, wamegawa vifaa vya kwa wanafunzi wenye mahitaji maalum katika shule zilizopo wilayani Ilala.
Akizungumza na waandishi wa habari Ofisa Elimu Msingi na Awali wa Halmashauri hiyo,Magreth Macha, amesema Wilaya ya Ilala ina shule zaidi ya 100 kati hizo shule zenye wanafunzi wa mahitaji maalum zipo 18.
Macha,amesema vifaa hivyo walivyogawa lvimetoka Serikali Kuu kwa ajili ya wanafunzi wa Wilaya ya Ilala wenye mahitaji maalum ikiwemo wa shule ya Uhuru Mchanganyiko,Buguruni Malapa,Mzambarauni na Chanika.
Pia ametoa wito kwa Walimu Wakuu wa shule hizo kutunza vifaa hivyo na vitumike kwa madhumuni yaliokusudiwa .
Huku akiitaka jamii yenye watoto wenye mahitaji maalum wasikae nyumbani badala yake wawapeleke shule wapate fursa ya kusoma elimu bila malipo.

More Stories
NMB yatambuliwa Marekani kwa ubunifu wa bima kidijitali
Ndoto zilizovunjika: Jinsi Mimba za utotoni zinavyowakatisha Wasichana elimu nchini Rwanda,Tanzania na Sudan Kusini
Miaka 50 ya Sabasaba Vodacom yadhihirisha kuchochea mageuzi ya kidigital nchini