May 22, 2024

Timesmajira

Gazeti Huru La Kila Siku

Halima Mdee, Wenzake
wachongewa kwa Samia

Na Mwandishi Wetu, TimesMajira,Online

MWENYEKITI wa BAWACHA Taifa, Sharifa Sulleman, amemuomba Rais Samia Suluhu Hassan, kuangalia kwa jicho la tatu kesi inayowakabili wabunge 19 wa chama hicho.

Sharifa ametoa kauli hiyo kupitia hotuba yake ya BAWACHA kwenye kongamano la Siku ya Wanawake Duniani, ambapo Rais Samia alikuwa mgeni rasmi.