Na Mwandishi Wetu, Timesmajira Online
Aliyekuwa Msemaji wa klabu ya Simba, Haji Manara
ametangaza rasmi kujiunga na Yanga jioni hii Jijini
Dar es salaam, na pia amesema amehamia klabu hiyo
pamoja na Familia yake.
Akizungumza mara baada ya kutambuishwa rasmi kwenye
Hotel ya Serena Jijini Dar es Salaam, Manara
amesema, anakwenda Yanga kutokana na kuwa na
viongozi watakaompa nafasi ya kuwasaidia.
“Nakwenda Yanga kwa sababu ina viongozi watakaonipa
nafasi ya kuwasaidia, nilibanwa mno, nilidhihakiwa
mno, sijawahi kuwa na matatizo na Simba,” amesema
Manara.
More Stories
Kasulu FC mabingwa mashindano Khimji 2025
Fainali Khimji cup kufanyika Februari 7,2025
Naibu Waziri wa Fedha abariki ujio mpya wa Bahati Nasibu