Na Joyce Kasiki,Timesmajira online,Dodoma
MAKAMU wa Rais Dkt.Philip Mpango ameoneshwa kuridhishwa na kazi inayofanywa na Shirika la Maendeleo ya Petroli nchini (TPDC) ya kuwaunganishia wananchi gesi asilia kutoka kwenye bomba kuu.
Akizungumza wakati wa kukagua mabanda kwenye Kongamano la Wanawake la Nishati safi ya kupikia, Dkt.Mpango amesema shirika hilo linafanya kazi nzuri ambayo itachangia wananchi kuachana na nishati chafu ya kupikia.
Hata hivyo amemwagiza Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika hilo Mussa Makame kuhakikisha wanaendelea kusambaza gesiasilia kwa wananchi huku akilitaka shirika hilo liangalie uwezekano wa njia za kulipatia pesa shirika kwa ajili kuliongezea nguvu katika utekelezaji wa majukumu yake.
Awali Mkurugenzi Mtendaji wa TPDC Makame amesema shirika hilo limeanza safari ya
kuwezesha wananchi wa Mikoa ya Lindi,Mtwara,Pwani na Dar es Salaam kutumia gesi asilia inayozalishwa hapa nchini.
Aidha amesema mpaka sasa wameshaunganisha takriban taasisi 13 zikiwemo baadhi ya magereza na shule pia wameunganisha wananchi 1500.
Hata hivyo Mkurugenzi huyo amesema changamoto kubwa wanayokabiliana nayo ni usambazaji wa gesi kwa bomba njia ambayo gharama yake ni kubwa huku akisema wanaangalia uwezekano wa kusambaza gesi asilia kwa njia ya mitungi ili kuwezesha wananchi wengi zaidi kuhama kwenye matumizi ya kuni na mkaa na badala yake waanze kutumia nishati safi ya kupikia.
More Stories
Kamati ya kudumu ya Bunge ya utawala,katiba na sheria yaridhishwa ujenzi soko Kariakoo
TRA Tanga yakusanya bil.178.3 kwa miezi sita
Wataalam Sekta ya utalii watakiwa kufanya kazi kwa uadilifu,kujituma na kuwa wabunifu