Na Penina Malundo,TimesMajira,Online
KATIBU Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Dkt. Bashiru Ally Kakurwa, ameongoza mapokezi ya kumpokea mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa tiketi ya CCM, Dkt. John Pombe Joseph Magufuli.

Mapokezi hayo, yamefanyika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Zanzibar leo tarehe 02 Oktoba, 2020 ambapo Dkt. Magufuli ameeleza kwa ufupi,
“Leo nimeingia hapa Zanzibar, nimeingia Zanzibar kwa ajili ya kuja kufanya kampeni, kwa wagombea wote wa Chama Cha Mapinduzi.”
Mgombea wa Urais wa CCM,Dkt. Magufuli anatarajiwa kufanya mkutano mkubwa wa kampeni kesho tarehe 03 Oktoba, 2020 katika viwanja vya Mnazi mmoja Mkoa wa Mjini.
Aidha Dkt.Magufuli anatarajia kufanya mkutano wa kampeni katika viwanja vya mnazi mmoja kesho ambapo atapata fursa ya kuonyesha maono yake ya ustawi wa Tanzania,Maisha ya Watu pamoja na namna atakavyoongoza ndani ya kipindi cha miaka mitano ijayo.
Ambapo ratiba ya mkutano huo utahudhuriwa na wasanii Mbalimbali ambao ni mkada wa chama hicho na kufatiwa na maelezo yake juu ya ilani yao ya Uchaguzi inavyosema katika kipindi cha miaka mitano ijayo.

More Stories
EWURA yatangaza bei ya mafuta
Msajili wa Hazina akutana na kufanya mazungumzo na viongozi wa EADB
Tanzania mwenyeji wa Mkutano wa 153 wa Umoja wa Mabunge Duniani