Na Mwandishi wetu, Timesmajira Online
Maafisa Waandamizi kutoka Shirika la Miliki Ubunifu Kanda ya Afrika (ARIPO), kwa kushirikiana na Maafisa Waandamizi kutoka Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA), wamefanya ziara ya kutembelea Mawakala sita (6) wa Tanzania waliopo jijini Dar es Salaam, kuona namna ambavyo wanasajili alama za biashara, huduma pamoja na kutoa hataza kwa wafanyabiashara na wavumbuzi wa Tanzania kupitia mfumo unaosimamiwa na ARIPO na kusikiliza changamoto wanazopitia Mawakala hao pindi wanaposajili kupitia mfumo.Â
BRELA inaendelea kuhamasisha wafanyabiashara kusajili Alama za Biashara na Huduma pamoja na kupata Hataza ili kupewe ulinzi wa Kisheria. Mawakala waliotembelewa ni Bowmans Tanzania, AKP Laws Advocates, FB Attorneys, NexLaw, Lexglobe IP Services na Crystal Associates.
More Stories
Makonda aipongeza CRDB kuimarisha utalii kwa kutoa nyenzo za ulinzi
Serikali kutenga bajeti ya vyombo vya habari
Watoto 194 wapewa mimba ndani ya mwezi mmoja