Taarifa zilizotufikia ni kuwa Mchungaji wa Kanisa la Warehouse Christian Center Peter Mitimingi amefariki dunia jana.
Mchungaji Mitimingi wa Kanisa la Warehouse Christian Center lililoko Africana, jijini Dar es Salaam, alikuwa Mkurugenzi Mtendaji wa huduma ya the Voice of Hope Ministry, Mshauri wa Saikolojia wa BLCCC
.
Alifahamika zaidi kwa mahubiri na mafundisho yake kuhusu mahusiano na maisha ya ndoa yaliyoenea zaidi kupitia Mitandao ya Kijamii.
Taarifa zaidi zitakujia muda si mrefu, fuatilia kupitia mtandao wa Timesmajira.co.tz

More Stories
Yas yazindua Mnara wa 5G Masasi
Wafanyabiashara wahimizwa kutumia nembo ya Tanzania
Tozo ya mafuta yaboresha barabara Mwanza