May 16, 2024

Timesmajira

Gazeti Huru La Kila Siku

Barty aongoza viwango vya tenis duniani kwa wanawake

ST. PETERSBURG, Florida

NYOTA wa tenis Ashleigh Barty, ambaye alishinda mashindaano ya tenis hivi karibuni Stuttgart nchini Ujerumani mwishoni mwa wiki, bado anaendelea kuwa nambari moja ulimwenguni kwa juma la 70 sasa, akiwa na alama 1,855 mbele ya Naomi Osaka, katika viwango vya WTA vilivyotolewa juzi.

Barty, mwenye umri wa miaka 25 raia wa Australia, ambaye hakushiriki mashindano yoyote mwaka jana kwa sababu ya wasiwasi wa Covid-19, amenufaika na mfumo wa mpito, uliowekwa kwa muda wa janga hilo, ikiruhusu wachezaji kuhesabu mashindano yao 16 bora kuanzia Machi 2019 badala ya mzunguko wa kawaida wa wiki 52.

Mchezaji huyo amesisitiza kuwa sifa zake za kushinda mataji matatu 2021. Hajapoteza kua mchezaji bora tangu alipopigwa na Mholanzi Kiki Bertens katika mchezo wa roboti huko Shenzhen mnamo 2019.

Kwa mara ya kwanza Karolina Muchova anaonekana kushika nambari 20 kwa ubora wakati Sorana Cirstea, ambaye alishinda taji lake la pili la mzunguko huko Istanbul siku ya Jumapili akipanda nafasi tisa hadi ya 58.

Wachezaji watano bora katika mchezo wa tenis duniani kwa upande wa wanawake

  1. Ashleigh Barty (Australia) alama 9655
  2. Naomi Osaka (Japan) alama 7800
  3. Simona Halep (Romania) alama 7050
  4. Sofia Kenin (Marekani) alama 5915
  5. Elina Svitolina (Ukrine) alama 5835