Na Mwandishi Wetu, Timesmajira Online
Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo. Balozi Dkt. Pindi Chana, ameshiriki kikao cha Kamati ya Ushauri ya Mkoa wa Njombe kilichohudhuriwa na viongozi na watendaji wa Idara na Taasisi mbalimbali za mkoa huo.
Balozi Dkt. Chana ametumia fursa hiyo kusisitiza Mikoa na Halmashauri zote nchini zitenge fedha za kukarabati na kujenga miundombinu kwa ajili ya shughuli za Utamaduni, Sanaa na Michezo.
Aidha, ametoa wito kwa viongozi wa Halmashauri na mikoa kote nchini waendelee kuunga mkono juhudi za Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan kuendeleza shughuli za Utamaduni, Sanaa na Michezo kutokana na umuhimu wake katika kukuza na kutoa fursa za ajira kwa vijana ambao ni wengi hapa nchini.
More Stories
Magwiji 27 wafuzu raundi ya tatu mashindano ya kumuenzi Lina
Mafanikio Wizara ya Ulinzi kwenye michezo miaka 60 ya muungano
Mbunge Bonnah agawa jezi za mashindano ya Bonah Cup 2024