October 5, 2024

Timesmajira

Gazeti Huru La Kila Siku

Kaimu Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri (TEF) Deodatus Balile, akifungua Mkutano Mkuu wa Tisa jijini Dodoma leo. Picha na TimesMajira Online

Balile awasaa wahariri kuzingatia maadili, taaluma yao

Na Joyce Kasiki, TimesMajira Online, Dodoma

KAIMU Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri (TEF) nchini, Deodatus Balile amewataka wahariri na waandishi wa habari kwa ujumla kusimamia maadili na taaluma yao badala ya kuingia kwenye mitego ya kutaka vyama vya siasa kushinda katika Uchaguzi Mkuu wa Oktoba mwaka huu.

Akizungumza Jijini Dodoma leo na waandishi wa habari mara baada ya ufunguzi wa Mkutano Mkuu wa TEF utakaofanyika kwa siku mbili ambapo pia utafanya mapitio ya utendaji wa vyombo vya habari mwaka uliopita na kuweka mipango ya mwaka huu Balile amesema,jukumu la mwandishi wa habari kulinda na kufuata misingi ya taaluma yake na siyo vinginevyo.

Amesema kipindi hiki cha uchaguzi ndio wakati ambao waandishi wa habari wanapaswa kufanya kazi kwa ufanisi huku wakitambua zipo sheria zinazowaongoza na zinafanya kazi.

“Kipindi hiki cha uchaguzi malalamiko ni mengi ,tusiyapuuze bali tuangalie namna ya kuyashughulikia ,lakini vyombo vya habari havipaswi kutumika kutukana wengine au kwa uchochezi,’ amesema Balile