Na Suleiman Abeid, Shinyanga
MKAZI wa Uzogore Kata ya Ibadakuli, Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga amejeruhiwa kwa kukatwa na kisu sehemu za ubavuni kulia na mkewe baada ya kutokea ugomvi kati ya wanandoa hao.
Tukio hilo ni la pili kutokea mjini hapa ndani ya wiki moja la wanawake kuwajeruhi waume zao.
Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Shinyanga, Debora Magiligimba amemtaja mwanaume aliyejeruhiwa kuwa ni Mpemba Gamba (48) na kwamba tukio hilo lilitokea saa sita usiku wa kuamkia jana baada ya kutokea ugomvi kati yake na mkewe aliyetajwa kwa jina la Suzana Richard mkazi wa Uzogore.
Amefafanua kuhusu tukio hilo, Kamanda Magiligimba alisema chanzo cha ugomvi kati ya wanandoa hao ni mwanamke kulazimisha kuendelea kuishi na mumewe baada ya kuwa amefukuzwa kwa kosa la kushindwa kumpikia mumewe.
Pata habari hii kwa kina kwenye Gazeti la Majira…
More Stories
NMB ‘yafunga ndoa’ na wanawake wanaomiliki shule, vyuo Tanzania
RC Mwanza afanya ziara ya kikazi katika mradi wa uwekezaji jengo la Hotel ya nyota tano wa NSSF
Wasichana vinara waiomba serikali kuondoa kodi kwenye taulo za kike