March 7, 2026

Timesmajira

Gazeti Huru La Kila Siku

Aida Haule achukua fomu kugombea Udiwani ataja vipambele vyake akishinda

Na Esther Macha,TimesmajiraOnline,Mbeya

MGOMBEA Udiwani kupitia chama cha Mapinduzi (CCM)Kata ya Utengule Usongwe Wilaya ya Mbeya,Aida Haule amechukua fomu ya kugombea nafasi hiyo huku akitaja vipambele vinne akishinda.

Ametaja vipaumbele hivyo kuwa ni pamoja kushirikiana na serikali pamoja na wananchi  ili kujenga Vyumba vya madarasa   na kuhakikisha Mji wa Mbalizi unakuwa Mamlaka kamili tofauti na sasa  ambapo  inatamkwa kwa maneno .

Akizungumza na waandishi wa habari  Agosti 19,2025 ,baada ya kuchukua Fomu ya kugombea Udiwani kata ya Utengule Usongwe amesema kata hiyo imekuwa na changamoto ya muda mrefu ya  kutokuwa na Mamlaka kamili na kusema mamlaka iliyopo ipo kwa kutamka lakini bado inaitwa kwa jina tu.

“Hii kata ina kilio cha muda mrefu hivyo natarajia viongozi wetu ngazi  ya  chama na  kitaifa iwafikirie  wananchi wa kata hii kwani mpaka sasa kuna kilometa mbili tu za  barabara ya lami,”amesema.