Na Agnes Alcardo, Timesmajira Online
NAIBU Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Bara, John Mongella, amewataka wanachama wa chama hicho kudumisha amani na utulivu kuelekea Uchaguzi Mkuu wa mwaka huu.

Akizungumza jijini Arusha kwa niaba ya Katibu Mkuu wa CCM, Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi, Mongella amewahimiza wana-CCM kuwa makini na kuepuka vishawishi vinavyoweza kusababisha vurugu.
Amesisitiza kuwa, huu ni wakati wa kuwa imara huku akieleza kuwa Tanzania ina heshima ya kipekee barani Afrika kutokana na utamaduni wake wa kudumisha amani na utulivu.


More Stories
Airtel  yaimarisha ushirikiano  wa Airtel Business Monthly Mug TournamentÂ
GF yaahidi kuendelea kuunga mkono maono ya Serikali
Mwanasheria Mkuu wa Serikali awataka TPBA kuwa wabunifu