Mitandao ya kijamii ya TikTok na WeChat inayomilikiwa na Wachina utazuiwa ndani ya siku 45 zijazo kama isipouzwa kwa Wamarekani ndani ya siku hizo.
Hayo yamebainishwa na Rais wa Marekani Donald Trump ambapo amepanga kuzuia mitandao hiyo Septemba 15, ikiwa haitauzwa.
Aidha, Wahusika wa mitandao hiyo wapo katika maongezi na kampuni ya kimarekani ya Microsoft.
Sababu za Rais Trump kuifunga mitandao hiyo imetokana na tuhuma za kuiba taarifa za watumiaji wake na kupeleka kwa Serikali za China ambapo hadi sasa TikTok ina watumiaji zaidi ya milioni 100 nchini Marekani

More Stories
Migogoro na uhamishaji  janga lakisiasa, kibinadamu barani Afrika
Wanasayansi Wafichua siri nzito kuhusu chanzo cha viazi vya chips
Gavu asisitiza kuimarisha ushirikiano Tanzania na China