Na Bakari Lulela, TimesMajira Online
MWANAMITINDO Hamisa Mobeto, ametambulishwa kuwa Balozi wa bidhaa ya tambi aina ya Spaghetti inayotengenzwa na kampuni ya Azania Group.
Mobeto ametambulishwa leo, Julai 26, 2024 jijini Dar es Salaam na Mkurugenzi wa Biashara wa kampuni hiyo, Joel Laizer na kufafanua kuwa bidhaa hiyo ina miezi sita tangu kuingizwa sokoni.
Akizungumza baada ya kutambulishwa, Mobeto alisema kuwa alikuwa akiitumia bidhaa hiyo Kwa kipindi kirefu na ni furaha kwake kuwa Balozi na anaamini atafanya vema kuhamasisha jamii kuzitumia.
“Naamini watanzania wataitumia kutokana a na ubora wa bidhaa tofauti na nyingine, hivyo nawaomba jamii kubwa wajitokeze kuitumia,”amesema Laizer
Awali Mkurugenzi, Laizer, alisema kuwa bidhaa hiyo inautofauti mkubwa na nyingine hivyo ni huu ndio wakati sahihi kuitumia.
Hii bidhaa inaradha nzuri na haikamatiki kama nyingine hivyo ubora wake ni mkubwa tofauti na nyingine,”amesema
More Stories
Tamasha la utamaduni mkoani Ruvuma lapamba moto, Rais Samia mgeni rasmi
TANAPA yazindua Twenzetu Kilele msimu wa nne
Shamrashamra maadhimisho ya miaka 60 JWTZ yaendelea