Na Mwandishi wetu, TimesMajira Online
Naibu Waziri wa Afya Dkt. Godwin Mollel amesema Serikali inayoongozwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan imetoa kiasi cha shilingi Bilioni 2.6 kuboresha huduma za afya ambapo katika kuboresha huduma hizo kuna ujenzi wa majengo ya mama na mtoto, jengo la upasuaji na jengo la maabara katika hospitali ya wilaya ya kiteto iliyopo mkoani Manyara.
Dkt Mollel ameeleza hayo leo wakati alipofanya ziara wilayani humo ya kukagua hali ya utoaji wa huduma za afya katika Hospitali ya Wilaya .
Dkt.Mollel amesema kuwa serikali inaendelea kuboresha huduma za afya ambapo mpaka sasa Wilaya ya kiteto imepokea Vifaa vya shilingi Milioni 185 kutoka Bohari ya Dawa ( MSD) na kusambazwa katika vituo vya kutolea huduma za afya wilayani humo.
More Stories
Mramba akagua jengo la Wizara ya Nishati Mtumba
Serikali yathamini mchango wa viongozi wa Dini kwenye maendeleo
Waziri Jafo awaasa wajumbe Bodi ya FCC kuwa waadilifu, waaminifu