October 6, 2024

Timesmajira

Gazeti Huru La Kila Siku

Raza achukua fomu kuwania ubunge Jimbo la Kiembe Samaki

Na Mwanadishi Wetu, TimesMajira Online, Zanzibar

MWANASIASA wa Zanzibar, Ibrahim Hassanali Raza, amechukua fomu za kuwania ubunge katika Jimbo la Kiembe Samaki.

Raza ambaye alikuwa mwakilishi aliyemaliza muda wake katika Jimbo la Kiembe Samaki amechukua fomu hiyo jana, JUlai 15 akiomba kuwania nafasi hiyo kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM).