Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli amemteua Dkt. Delphine Diocles Magere kuwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Pwani.
Dkt. Magere anachukua nafasi ya Bi. Theresia Mmbando ambaye amestaafu.
Kabla ya uteuzi huo, Dkt. Magere alikuwa Ofisi ya Rais akishughulikia masuala ya uchumi.
Wakati huo huo, Mhe. Rais Magufuli amemteua Bw. Dunstan Kyobya kuwa Mkuu wa Wilaya ya Mtwara, Mkoani Mtwara.
Bw. Kyobya anachukua nafasi ya Bw. Evod Mmanda aliyefariki Dunia tarehe 27 Aprili, 2020.
Kabla ya uteuzi huo, Bw. Kyobya alikuwa Mshauri wa Rais katika masuala ya sheria.
Uteuzi wa viongozi hao unaanza leo tarehe 06 Mei, 2020.
Imetolewa na Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU

More Stories
DCEA yateketeza ekari 603 mashamba ya bangi Mvomero
Airtel Money School Pay yarahisisha ulipaji wa Ada
Yas yaongeza kasi kuchochea uchumi wa buluu Zanzibar