Na Mwandishi Wetu, TimesMajira Online
MUIGIZAJI wa filamu na Mjasiriamali hapa nchini Shamsa Ford, ametoa ujumbe mzito kwa jamii na kuwataka kuombeana mema pindi binadamu mwenzao anapopata matatizo ya kudunia.
Akitoa ujumbe huo kupitia kwenye Ukurasa wake wa Instagram Shamsa amesema, kuna kipindi mwanadamu huwa anapitia changamoto mbalimbali hivyo ni vyema kumpa moyo pindi anapotwa na mitihani.
“Huwezi kuelewa maumivu ya mwenzio mpaka yakukute. Tuishi kwa kuoneana huruma na kuombeana mema jamani, mwenzako anapopitia mitihani tusiwe wa kuhukumu hata wewe unaweza ukapitia, kama bado unaishi duniani ni kumuomba tu Mungu atuepushe na mabalaa hakuna anayeijua kesho yake,” ameandika Shamsa.
More Stories
Wajumbe wa Mkutano Mkuu wa CCM wakiburudika kusubiri Uzinduzi Ilani ya CCM 2025-2030
Mwanamitindo Millen Magese apewa kibali kuandaa Miss Universe Tanzania 2025
Pacha Milionea waja na truck mpya “Nyumbani”