Na Mwandishi Wetu, TimesMajira Online
MUIGIZAJI wa filamu na Mjasiriamali hapa nchini Shamsa Ford, ametoa ujumbe mzito kwa jamii na kuwataka kuombeana mema pindi binadamu mwenzao anapopata matatizo ya kudunia.
Akitoa ujumbe huo kupitia kwenye Ukurasa wake wa Instagram Shamsa amesema, kuna kipindi mwanadamu huwa anapitia changamoto mbalimbali hivyo ni vyema kumpa moyo pindi anapotwa na mitihani.
“Huwezi kuelewa maumivu ya mwenzio mpaka yakukute. Tuishi kwa kuoneana huruma na kuombeana mema jamani, mwenzako anapopitia mitihani tusiwe wa kuhukumu hata wewe unaweza ukapitia, kama bado unaishi duniani ni kumuomba tu Mungu atuepushe na mabalaa hakuna anayeijua kesho yake,” ameandika Shamsa.
More Stories
Tamasha la utamaduni mkoani Ruvuma lapamba moto, Rais Samia mgeni rasmi
TANAPA yazindua Twenzetu Kilele msimu wa nne
Shamrashamra maadhimisho ya miaka 60 JWTZ yaendelea