August 13, 2026

Timesmajira

Gazeti Huru La Kila Siku

Yanga yatwaa Ngao ya Jamii ,Simba chali

NAIBU Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Hamis Mwinjuma, ameungana na viongozi mbalimbali pamoja na mashabiki wa soka kushuhudia mchezo wa Ngao ya Jamii uliowakutanisha watani wa jadi, Simba na Yanga, Agosti 12 2026.

Mchezo huo uliokuwa ukisubiriwa kwa hamu na mashabiki wa soka nchini, umemalizika kwa Yanga kuibuka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Simba na hivyo kutwaa taji la Ngao ya Jamii ambalo wamekabidhiwa na Waziri wa Mambo ya ndani ya nchi, Mhe. Patrobas Katambi