March 7, 2026

Timesmajira

Gazeti Huru La Kila Siku

TMA yatoa utabiri wa hali ya hewa kwa saa 24 zijazo.

Na Mwandishi Wetu, Timesmajira Online-Dar

Kwa Mujibu wa taarifa ya Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania(TMA), imeeleza kuwa vipindi vifupi vya mvua kubwa inatazamiwa katika mikoa ya Arusha,Kilimanjaro,Manyara Rukwa,Songwe ,Mbeya ,Iringa ,Njombe ,Morogoro,Lindi,na Mtwara.

Ambapo TMA imesema Visiwa vya Unguja na Pemba ,Mikoa ya Dodoma,Singida ,Tanga, Dar-es-Salaam,Kigoma ,Tabora,Katavi,mikoa ya Pwani ikijumuisha Visiwa vya Mafia,Mikoa ya Geita,Mwanza na Shinyanga,itakuwa na hali ya mawingu mvua ngurumo katika maeneo machache na vipindi vifupi vya jua.

Taarifa hiyo imeeleza mikoa ya Mara na Simiyu,Morogoro,Lindi na Mtwara , Arusha ,Kilimanjaro na Manyara, Rukwa ,Songwe, Mbeya,Iringa,Njombe,na Ruvuma itakuwa na hali ya mawingu mvua na ngurumo katika baadhi ya maeneo na vipindi vifupi vya jua.

Mwisho