July 5, 2026

Timesmajira

Gazeti Huru La Kila Siku

WMA yazidi kuwafikishia elimu Wajasiriamali

Na.Mwandishi wetu,Timesmajira

Katika siku ya nane ya Maonesho ya Biashara ya Kimataifa maarufu kama SabaSaba, yanayoendelea jijini Dar es Salaam, Wakala wa Vipimo (WMA) imeendeleza mkakati wake wa kuwatembelea wajasiriamali na kuwapatia elimu kuhusu matumizi sahihi ya vipimo.

Zoezi la utoaji elimu ya vipimo kwa wajasiriamali linaenda sambamba na kuhudumia wadau mbalimbali wanaotembelea banda la WMA katika Maonesho hayo ya SabaSaba.

Lengo ni kuhakikisha elimu na huduma mbalimbali za ki-vipimo zinafikishwa kwa wadau wengi kadri iwezekanavyo.