Na Bakari Lulela, Timesmajira Online,Dar
MFUKO wa Utamaduni na Sanaa Tanzania umeendesha warsha maalumu yenye lengo la kuwasaidia wasanii kuandaa na kutengeneza kazi bora,ili kunufaika na milabaha ama kazi zao ndani ya nchi.
Takwimu zinaonesha kuwa tasnia hiyo inachangia pato la Taifa kwa kiasi cha asilimia 17.1 ukilinganisha na sekta nyingine nchini hivyo kuwa eneo muhimu katika kuchochea shughuli za maendeleo.
Akizungumza jijini Dar-es-Salaam, Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo,Gerson Msigwa amesema wasanii ni nguzo muhimu katika maendeleo ya nchi hivyo inabidi kuangaliwa kwa macho mawili.
“Warsha hii ni muhimu kwa makundi haya ya wasanii ili kuweza kuwatengenezea mazingira yenye kuzifanya kazi zao ziwe zenye ubora machoni mwa watanzania kupitia serikali,” amesema Msigwa
Amesema,warsha hiyo ilijumuisha mafunzo mbalimbali ya kazi za sanaa na namna ya wasanii kupata mikopo wezeshi,ambayo itakwenda kuboresha kazi zao ama shughuli wazifanyazo kwa manufaa yao na serikali kwa ujumla.
Hata hivyo warsha hiyo ilijumuisha wasanii mbalimbali ikiwemo maigizo, wasanii bongo fleva, washairi na watunzi wa vitabu, waandishi wa script pamoja na waimbaji wa injili na wa taarabu.
More Stories
BAKWATA yawazawadia washindi wakuhifadhi Qur’an
Chalamila:Dar ni salama,aelezea mafanikio na mipango ya maendeleo ya Mkoa
Ulaji vyakula vya aina moja,umri vyatajwa ongozeko la matatizo ya macho Mbeya