Na Moses Ng’wat,TimesMajira Online. Songwe
WATU wenye ulemavu mkoani Songwe wameiomba Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), kuweka mazingira yatakayowezesha kutimiza haki yao kikatiba ya kupiga kura bila kuwepo kwa vikwazo.
Wametoa ombi hilo jana katika semina maalumu iliyoandaliwa na NEC kwa wadau wa uchaguzi mkoani hapa.
Wamesema kutokuwepo kwa mazingira rafiki kwa makundi ya watu wenye ulemavu ikiwemo uchaguzi wa mwaka huu, kunaweza kuwa chanzo cha wao kutowapata viongozi ambao watasimamia maslahi yao.
Mmoja wa walemavu hao, Martin Tembo ambaye ni mlemavu wa viungo amesema walemavu wanapaswa kupewa kipaumbele ikiwemo kuweka mazingira wezeshi yatakayosaidia wao kupiga kura bila kupata usumbufu wowote.
“Changamoto inaweza isiwe walemavu kapatiwa mahitaji yao muhimu, bali ni namna gani watashiriki kupata viongozi watakaosaidia kuelewa umuhimu wa kundi hilo na kupigania maslahi yao,” amesisitiza Tembo.
More Stories
Kiongozi wa Mwenge awataka RUWASA kukamilisha mradi wa maji kwa wakati Kilindi
Balozi Nchimbi aongoza waombolezaji kumuaga Mzee Mongella
Ahukumiwa kunyongwa hadi kufa kwa kumuua mama yake mzazi