Na Mwandishi wetu,Timesmajira,Online
Waziri Mkuu wa Tanzania, Kassim Majaliwa ameweka jiwe la msingi la mradi wa ujenzi wa Chuo cha Ufundi Stadi cha Wilaya ya Ruangwa mkoani Lindi.
Mradi huo unatekelezwa na Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa kwa kusimamiwa na Mshauri Elekezi, Chuo cha Ufundi Arusha (ATC), kwa gharama ya shilingi bilioni 2.2 chini ya Mradi wa Kukuza Elimu na Ujuzi kwa Kazi zenye Tija (ESPJ).
Chuo hicho ambacho kinatarajia kukamilika mwezi Disemba 2021, kitakuwa na uwezo wa kudahili wanafunzi 560 kwa mwaka katika fani za ufundi umeme, Useremala, Uungaji na Uchomeleaji vyuma, Uashi, Ushonaji na Mitindo ya Mavazi, Usindikaji Vyakula na Tehama .
More Stories
BAKWATA yawazawadia washindi wakuhifadhi Qur’an
Chalamila:Dar ni salama,aelezea mafanikio na mipango ya maendeleo ya Mkoa
Ulaji vyakula vya aina moja,umri vyatajwa ongozeko la matatizo ya macho Mbeya