Na Dotto Mwaibale,TimesMajira Online
MUUNGANO wa Maaskofu zaidi ya 15 na Wachungaji 100 mwanzoni mwa wiki wamezindua kitabu kinachoelezea uongozi uliotukuka wa Rais Dkt. John Magufuli.
Kitabu hicho kimeandikwa na Mtendakazi katika Shamba la Bwana, Restoration Bible Church Kariakoo jijini Dar es Salaam.
Uzinduzi wa kitabu hicho kiitwacho Uongozi Uliotukuka, JPM ni Kiongozi wa Kisiasa na Kiroho, uliofanyika jijini Dar es Salaam, uliongozwa na Askofu Mkuu wa Makanisa ya Naioth Gospel Assemblies of God, ambaye pia ni Katibu Mkuu mstaafu wa Baraza la Maaskofu wa Kipentekoste Tanzania, Dkt. David Mwasota.
Dkt. Mwasota amesema, lengo la kuandikwa kitabu hicho ni kutazama uongozi wa Rais Magufuli kwa pande za kisiasa na kiroho.
Askofu huyo amesema katika utendaji kazi wake, Magufuli anamtegemea Mungu hivyo kumfanya aonekane anaiongoza nchi kwa upande wa kiroho.

More Stories
TAMWA yakumbusha jamii kupinga ukatili wa kijinsia kuelekea siku ya wanawake Duniani
Wanawake washauriwa kuchangamkia fursa za uchumi
Aida:Wanawake wakipata haki zote itapunguza migogoro