Na Esther Macha, Timesmajira Online Mbeya
MAHAKAMA ya Wilaya ya Chunya Mkoani Mbeya imewahukumu kifungo cha Maisha jela wakazi wawili wa wilaya hiyo kwa makosa ya kubaka na kulawiti watoto wadogo wa kike.
Hukumu hiyo imetolewa na Hakimu Mfawidhi wa Mahakama ya Wilaya Chunya James Mhanuzi machi 5,2025 na Mwendesha mashitaka wa Serikali wakili Mwajabu Tengeneza .
Mshitakuwa wa kwanza Antony Mwangoka (53) mkazi wa Mbugani Chunya alimbaka na kumlawiti mtoto mwenye (9).
Mshitakiwa huyo alitenda kosa hilo Disemba 17,2024 katika Kijiji cha Mbugani Wilayani Chunya mkoani Mbeya.
Amesema kuwa mshitakuwa huyo alikamatwa Disemba 22, 2024 na kufikishwa mahakamani na kutiwa hatiani kwa makosa mawili ya kubaka na kulawiti
Mama mzazi wa mhanga alibaini tukio hilo wakati akifua nguo za ndani za mtoto wake baada ya kukuta zimechafuka na alipomchunguza mtoto wake alibaini kubakwa na kulawitiwa na Anthony Mwangaka.
Mkazi mwingine wa kibaoni Chunya aitwaye Said kandonga (60)amehukumiwa kifungo cha Maisha gerezani kwa kosa la kumbaka mtoto wa miaka (8).
Hukumu hiyo imetolewa na Hakimu Mfawidhi wa Mahakama ya Wilaya Chunya
James Mhanuzi na Mwendesha mashitaka wa Serikali wakili Mwajabu Tengeneza Aprili Mosi, Mwaka huu
Mshitakiwa alitenda kosa hilo Septemba 16, 2024 katika Kijiji cha Kibaoni Wilayani Chunya na alikamatwa Oktoba 02, 2024 na kufikishwa mahakamani ambapo alitiwa hatiani kwa kosa la kubaka.
Siku ya tukio Mshitakiwa aligundua kuwa nyumbani kwa Mhanga mzazi wake hayupo ndipo aliingia ndani ya nyumba kisha kumbaka Mhanga na wakati anaendelea kutenda kosa hilo alikutwa na mama mzazi wa mtoto huyo ambaye alitoa taarifa Polisi ndipo ulifanyika msako na kufanikiwa kumkamata mtuhumiwa ambaye alihojiwa na kufikishwa mahakamani ambapo alitiwa hatiani.
More Stories
Chalamila:Dar ni salama,aelezea mafanikio na mipango ya maendeleo ya Mkoa
Ulaji vyakula vya aina moja,umri vyatajwa ongozeko la matatizo ya macho Mbeya
Kenya,Uganda zaanzisha mradi wa uendelezaji rasilimali za maji Angololo