BARAZA la Wazee wa Wilaya ya Kahama (UWAKA), wameiomba serikali kuitungia sheria sera yao itakayoelekeza katika utekelezaji wake kisheria.
Ombi hilo limetolewa juzi na Katibu UWAKA, Paul Ntelya ambapo alisema sheria hiyo itungwe ili ielekeze utekelezaji katika mambo ya msingi juu yao.
Ntelya amesema sera ya wazee ipo kwa miaka 17 toka mwaka 2003, lakini hadi sasa haina sheria yoyote inayoelekeza utekelezaji wake kisheria.
“Sera yetu ipo toka mwaka 2003 hadi sasa haina sheria yoyote, sasa imefika wakati naiomba serikali itunge sheria itakayoelekeza utekelezaji wake katika mambo ya msingi kwenye kuwahudumia wazee,” amesema Ntelya.
Ntelya amesema katika moja ya sehemu ya sera hiyo, inasema wazee watalipwa pensheni lakini hadi sasa utekelezaji wake, umekuwa haupo kwa sababu ya kutokuwepo kwa sheria yoyote inayoelekeza hivyo.
More Stories
Mume adaiwa kuua mke kikatili
Mhandisi Mramba:Umeme wa Jotoardhi kuunganishwa kwenye gridi ya Taifa ifikapo 2030
Watumishi wa Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali watakiwa kuendelea kuzingatia maadili ya utumishi wa umma