October 5, 2024

Timesmajira

Gazeti Huru La Kila Siku

Wanafunzi watatu St. Mary’s Mazinde Juu wapata Scolarship ya Samia

Na Yusuph Mussa, TimesMajira Online, Lushoto

WANAFUNZI watatu kati ya saba walioingia kwenye kumi bora kitaifa kidato cha sita mwaka 2022 ambao walishika nafasi ya sita, saba na nane kutoka Shule ya Sekondari ya Wasichana ya St. Mary’s Mazinde Juu, wamepata Scolarship ya Rais wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Pia, wanafunzi wanne kati ya hao akiwemo mshindi namba moja (Tanzania One) Chatherine Alphonce Mwakasege na wenzake walioshika nafasi ya pili, nne na tano, wao wamepata Scolarship ya Benki Kuu ya Tanzania (BoT).

Lakini pia shule hiyo imeendelea kuwa tishio nchini baada ya wanafunzi wake 140 kati ya 149 waliofanya mtihani wa Taifa wa kidato cha nne 2022, kupata daraja la kwanza (division one) na tisa kupata daraja la pili, huku kukiwa hakuna daraja la tatu, nne wala sifuri.

Hayo yalisemwa Februari 11, 2023 na Mkuu wa Shule ya Sekondari ya Wasichana St. Mary’s Mazinde Juu iliyopo Magamba, Wilaya ya Lushoto mkoani Tanga Mtawa Evetha Kilamba.

Ni kwenye mahafali ya 26 ya kidato cha sita ya shule hiyo, ambapo wanafunzi 286 walihitimu masomo ya ngazi hiyo.

“Bado tumeendelea kuaminika kwenu wazazi kwa kuwa tunaendelea kusimama vizuri kitaaluma.”

Tangu mwaka 2011, shule yetu imekuwa ikifanya vizuri kwenye matokeo ya kidato cha sita.

Kwa mfano mwaka 2022 wanafunzi waliomaliza walikuwa 296, ambapo daraja la kwanza walikuwa 256, daraja la pili 38, daraja la tatu mmoja, na hakukuwa na daraja la nne wala ziro.

“Katika matokeo hayo, shule ilishika nafasi ya 12 kitaifa, na nafasi ya pili kimkoa, ambapo wanafunzi saba waliingia kumi bora kitaifa. Na kati ya hao, wanne akiwemo aliyeshika nafasi ya kwanza kitaifa yaani Tanzania One Catherine Alphonce Mwakasege, wamepata Scolarship ya Benki Kuu ya Tanzania (BoT). Na wengine watatu wamepata Scolarship ya Mama Samia Suluhu Hassan” alisema Kilamba.

Kilamba aliwataja wanafunzi hao saba na nafasi zao kwenye mabano, Catherine Mwakasege (mwanafunzi wa kwanza kitaifa- PCB), Lucy Magashi (nafasi ya pili kitaifa- PCB), Minael Mgonja (nafasi ya nne kitaifa- PCB), na Norah Kidjout (nafasi ya tano kitaifa- PCB), hao wanasomeshwa na BoT.

Wanaosomeshwa na Rais Dkt. Samia ni Jenipher Chuwa (nafasi ya sita kitaifa- PCB), Pauline Mabamba (nafasi ya saba kitaifa- PCM) na Rachel Moshy (nafasi ya nane kitaifa- PCM).

Pia katika kumi bora ya wasichana kitaifa ya kidato cha sita 2022, Dina Ngiga (PCB) alishika nafasi ya nane, na Lisa Assey (EGM) alishika nafasi ya sita kwenye kumi bora kitaifa katika mchepuo wa sanaa.

“Kwa kidato cha nne mwaka 2022 walikuwa wanafunzi 149, ambapo daraja la kwanza ni 140 na daraja la pili ni tisa, na hakuna daraja la tatu, nne wala sifuri.”

Kwa utaratibu mpya, hakuna upangaji uliofanyika kuonesha nafasi ya shule, ila wapo waliofanya vizuri zaidi kwa kupata daraja la kwanza ya pointi saba mpaka tisa.

Wanafunzi 39 walipata pointi saba, wanafunzi 16 wakapata pointi nane (8), na wanafunzi 15 walipata pointi tisa.”Katika mtihani huo kuna wanafunzi wetu ambao wamepata ufaulu wa juu kwa kupata alama “A” katika masomo yote, mfano mwanafunzi wetu Khadija Hassan Mmuni, yeye ni mmoja wa wanafunzi wenye “A” zote” alisema Kilamba.

Kilamba amelishukuru Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC) kwa kutambua mchango wa shule zinazosimamiwa na Kanisa Katoliki, ambapo katika utambuzi huo, Shule ya Sekondari ya Wasichana ya St. Mary’s Mazinde Juu imetajwa na TEC kuwa imefanya vizuri kwa kupata Daraja A ambayo ni Excellent.

Mkuu wa Shule ya Sekondari ya Wasichana St. Mary’s Mazinde Juu iliyopo Magamba, Wilaya ya Lushoto mkoani Tanga Mtawa Evetha Kilamba akizungumza kwenye mahafali ya 26 ya kidato cha sita ya shule hiyo, ambapo wanafunzi 286 walihitimu masomo ya ngazi hiyo. (Picha na Yusuph Mussa).
Mwenyekiti wa Bodi ya Shule ya Sekondari ya Wasichana St. Mary’s Mazinde Juu iliyopo Magamba, Wilaya ya Lushoto mkoani Tanga Dkt. Kandi Lussingu akizungumza kwenye mahafali ya 26 ya kidato cha sita ya shule hiyo, ambapo wanafunzi 286 walihitimu masomo ya ngazi hiyo.
Mkuu wa Masista wa Shirika la Mama wa Usambara (COLU) Mtawa Gaspara Kashamba akizungumza kwenye mahafali ya 26 ya kidato cha sita ya Shule ya Sekondari ya Wasichana St. Mary’s Mazinde Juu, ambapo wanafunzi 286 walihitimu masomo ya ngazi hiyo. Wengine ni Mkuu wa Shule hiyo Evetha Kilamba (kushoto), na kulia ni Meneja na muanzilishi wa Shule hiyo mwaka 1989 Padre Damian Milliken (OSB) ambayo inamilikiwa na Jimbo Katoliki la Tanga, na imekuwa ikiongozwa na COLU. (Picha na Yusuph Mussa).
Mkuu wa Shule ya Sekondari ya Wasichana St. Mary’s Mazinde Juu iliyopo Magamba, Wilaya ya Lushoto mkoani Tanga Mtawa Evetha Kilamba (wa tatu kulia) akiongoza meza kuu kuimba wimbo wa Uzalendo kwenye mahafali ya 26 ya kidato cha sita ya shule hiyo, ambapo wanafunzi 286 walihitimu masomo ya ngazi hiyo. (Picha na Yusuph Mussa).
Mhitimu wa kidato cha sita Shule ya Sekondari ya Wasichana St. Mary’s Mazinde Juu Floraspera Leon akisoma risala kwenye mahafali ya 26 ya kidato cha sita ya shule hiyo, ambapo wanafunzi 286 walihitimu masomo ya ngazi hiyo. (Picha na Yusuph Mussa).
Sehemu ya wahitimu wa kidato cha sita Shule ya Sekondari ya Wasichana St. Mary’s Mazinde Juu wakiwaongoza wenzao kuimba wimbo wa kuaga. Ni kwenye mahafali ya 26 ya kidato cha sita ya shule hiyo, ambapo wanafunzi 286 walihitimu masomo ya ngazi hiyo. (Picha na Yusuph Mussa).
Wahitimu wa kidato cha sita Shule ya Sekondari ya Wasichana St. Mary’s Mazinde Juu wakiimba wimbo wa kuaga. Ni kwenye mahafali ya 26 ya kidato cha sita ya shule hiyo, ambapo wanafunzi 286 walihitimu masomo ya ngazi hiyo. (Picha na Yusuph Mussa).
Kwa mara ya kwanza, Shule ya Sekondari ya Wasichana St. Mary’s Mazinde Juu imekuwa na Brass Band yake. Ni baada ya kununua vyombo, na kuachana kukodisha. Wanafunzi wa kidato cha kwanza na pili wa shule hiyo, wamekabidhiwa jukumu la bendi hiyo, na hapo wanapiga matarumbeta kuwasindikiza viongozi jukwaani. Ni kwenye mahafali ya 26 ya kidato cha sita ya shule hiyo, ambapo wanafunzi 286 walihitimu masomo ya ngazi hiyo. (Picha na Yusuph Mussa).
Askofu wa Kanisa la KKKT Dayosisi ya Kaskazini Mashariki Dkt. Msafiri Mbilu (kushoto) akiwa kwenye mahafali ya 26 ya kidato cha sita ya Shule ya Sekondari ya Wasichana St. Mary’s Mazinde Juu. Ni kwa mara ya kwanza Askofu wa Dayosisi hiyo anaalikwa kwenye mahafali hayo, ambapo wanafunzi 286 walihitimu masomo ya ngazi hiyo. (Picha na Yusuph Mussa).
Wanafunzi wa Shule ya Mahitaji Maalumu ya Irente, Lushoto ambayo inamilikiwa na Kanisa la KKKT Dayosisi ya Kaskazini Mashariki, ni sehemu ya waalikwa kwenye mahafali ya 26 ya kidato cha sita Shule ya Sekondari ya Wasichana St. Mary’s Mazinde Juu iliyopo Magamba, Wilaya ya Lushoto mkoani Tanga. Katika kuchangia maendeleo ya shule hiyo ya wasichana kwa ajili ya ujenzi wa miundombinu, pia wadau waliichangia shule hiyo ya Irente zaidi ya sh. milioni nne (4). (Picha na Yusuph Mussa).