March 7, 2026

Timesmajira

Gazeti Huru La Kila Siku

Wairata:Nikipewa ridhaa nitaboresha miundombinu Kivule

Na Heri Shaaban, Timesmajira Online -Kivule

Mwanasheria Anita Waitara mtiania nafasi ya Ubunge,ambaye ni mmoja ni miongoni mwa watakaopigiwa kura za maoni ndani ya Chama cha Mapinduzi (CCM),ameahidi kuboresha miundombinu ndani ya Jimbo la Kivule,endapo atapata ridhaa ya kupeperusha bendera ya chama hicho katika uchaguzi mkuu mwaka huu

Akizungumza wakati wa kuomba kura za maoni ndani ya CCM Kata ya Majohe jimboni Kivule,Waitara, amesema, atabadirisha jimbo hilo liwe la kisasa kwa kuleta maendeleo katika huduma za jamii.

“Kwa taaluma mimi ni Mkemia pia Mwanasheria, miaka 30 sasa naishi kwenye Jimbo hili,na changamoto za Kata ya Majohe nazifahamu ikiwemo miundombinu ya barabara, hivyo mkinichagua nitashirikiana na Serikali kuboresha miundombinu yote ikiwemo ya sekta ya afya,elimu ikiwa ni pamoja na kujenga shule za mchepuo wa kiingereza pamoja na kuongeza vifaa tiba,”.

Pia amesema,tashirikiana na Serikali kutafuta wafadhili pamoja na kusimamia mazingira kwa kuleta magari ya kubeba takataka kwa kila Kata ili mji wa Majohe na Jimbo hilo liweze kuwa safi.

Aidha atachimba visima ili aweze kumtua mama ndoo kichwani sambamba nakuleta bima ya afya kwa wazee kwa ajili ya matibabu na kushirikiana na taasisi zote za dini pamoja na kuwainganisha vijana katika kuleta maendeleo ya kiuchumi.

” Mimi ni mwanamke nitasimama na wanawake wezangu katika mikopo ya asilimia kumi ambayo inatolewa ngazi ya Halmashauri,ili waache kukopa kausha damu sambamba na kuunda vikundi vya wanawake na bodaboda,”.