September 18, 2024

Timesmajira

Gazeti Huru La Kila Siku

Wahasibu waaswa kufanya kazi kuendana na ukuaji wa teknolojia

Na Iddy Lugendo, Timesmajira Online

WAZIRI wa nchi ofisi ya Rais Ikulu Serikali ya Mapinduzi Zanzibar CPA Jamaal Kasim Ally, amewaagiza wahasibu na wakaguzi wa hesabu nchini kufanya kazi kwa kuendana na ukuaji wa sayansi na teknolojia ili kuharakisha utoaji wa taarifa za mahesabu kwa umma.

Akizungumza jijini Dar es Salaam katika kilele cha maadhimisho ya miaka 50 ya Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi Tanzania (NBAA), ambapo amewataka wahasibu kushirikiana na serikali mtandao ili kuendana kasi teknolojia ya habari na mawasiliano.

Hata hivyo amewasihi wahasibu na wakaguzi kufanya kazi kwa uadilifu na kuzingatia miiko na maadili ya kazi yao kwani taaluma hiyo ni muhimu katika uchumi wa nchi na ustawi wa maendeleo ya nchi.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi Tanzania Prof. Sylivia Temu amesema bodi hiyo imejipanga kwa miaka miwili ijayo kuanza kutoa taarifa za uendelevu wa taasisi za umma na binafsi itakayoonyesha faida na athari zake kwa jamii.

Waziri wa nchi Ofisi ya Rais Ikulu – Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar CPA Jamal Kassim Ali akikata utepe kuashiria kuzindua kitabu cha hitoria ya miaka 50 ya Bodi ya  Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu  Tanzania(NBAA)  wakati wa mkutano mkuu wa mwaka 2022 pamoja na maadhimisho ya miaka 50 yaliyofanyika katika hoteli ya APC Bunju jijini Dar es Salaam.
Waziri wa nchi Ofisi ya Rais Ikulu – Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar CPA Jamal Kassim Ali(kushoto) akimkabidhi tuzo Mwenyekiti wa Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu Tanzania (NBAA), CPA. Prof. Sylvia S. Temu (kulia) Katikati ni Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu (​NBAA), CPA Pius A. Maneno, wakati wa ufunguzi wa mkutano mkuu wa mwaka 2022 pamoja na maadhimisho ya miaka 50 ya Bodi ya  Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu  Tanzania(NBAA)  yaliyofanyika Novemba 30, 2022 katika hoteli ya APC Bunju jijini Dar es Salaam.
Waziri wa nchi Ofisi ya Rais Ikulu – Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar CPA Jamal Kassim Ali(katikati) akimkabidhi tuzo Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu (​NBAA), CPA Pius A. Maneno(kulia) pamoja na kupongezwa na Mwenyekiti wa Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu Tanzania (NBAA), CPA. Prof. Sylvia S. Temu(kushoto) wakati wa ufunguzi wa mkutano mkuu wa mwaka 2022 pamoja na maadhimisho ya miaka 50 ya Bodi ya  Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu  Tanzania(NBAA)  yaliyofanyika Novemba 30, 2022 katika hoteli ya APC Bunju jijini Dar es Salaam.
Washindi wa Mpira wa miguu kuanzia mshindi wa kwanza mpaka wa tatu walioshiriki kwenye mashindano ya maadhimisho ya miaka 50 ya Bodi ya Wahasibu na Wakaguzi wa hesabu Tanzania wakipokea vikombe vyao wakati wa ufunguzi wa mkutano mkuu wa mwaka 2022 pamoja na maadhimisho ya miaka 50 ya Bodi ya  Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu  Tanzania(NBAA)  yaliyofanyika Novemba 30, 2022 katika hoteli ya APC Bunju jijini Dar es Salaam.Â