Na Mwandishi Wetu, Timesmajira Online
WAATHIRIKA wa maporomoko ya maji na tope, wameishukuru serikali kwa jitihada wanazozifanya ikiwemo msaada wa tiba ya kisaikolojia ili kuwanusuru na hali waliyonayo kwa sasa.
Maporomoko hayo yalitokea katika kijiji cha Ganana wilayani Hanang mkoa wa Manyara, ambapo baadhi yao wakiwemo wanafunzi waliopoteza wazazi na kupata athari ya afya ya akili kutokana na msongo wa mawazo.

Mwenyekiti wa Kitongoji cha Ganana, Maiko Henda amesema baadhi ya changamoto zinazowakabili kwa sasa ni afya ya akili kutokana na wahanga wengi wengi kupoteza wazazi, ndugu na mali.
Aidha, Serikali imeendelea kutoa huduma mbalimbali za kijamii ikiwemo kutuma timu za wataalamu wakiwemo wa tiba na saikolojia kutoka Wizara ya Afya na Tamisemi.
Lengo ni kufanya tathimini ya athari zilizojitokeza pamoja na utoaji wa elimu kuhusu masuala mbalimbali kwa waathirika hao.



More Stories
Bilioni 7 kuwainua vijana 308 sekta ya uvuvi
Clara:Miaka 50 ya Sabasaba fursa mpya za Biashara na Uwekezaji
Usajili wa Laini za Simu: Jilinde Dhidi ya Kutumiwa Vibaya kwa Utambulisho Wako