Na Penina Malundo, Timesmajira
MAMLAKA ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) inatoa taarifa ya uwepo wa kimbunga “IALY” katika Bahari ya Hindi kaskazini mwa kisiwa cha Madagascar.
Taarifa iliyotolewa kwa umma na Mamlaka hiyo Leo,imesema mifumo ya hali ya hewa inaonesha kuwa kimbunga hicho kitaendelea kusalia katika Bahari ya Hindi katika eneo kati ya Madagascar na visiwa vya Shelisheli kwa siku nne zijazo kabla ya
kuanza kupungua nguvu.
Imesema kuwa kutokana na umbali kutoka nchini, kimbunga hicho hakitarajiwi kuwa na athari za moja kwa moja katika kusababisha ongezeko la mvua nchini.
Taarifa hiyo imesema vipindi vya upepo mkali na
mawimbi makubwa vinaweza kujitokeza katika Bahari ya Hindi.
“TMA inatoa ushauri kwa watumiaji wa bahari na Wananchi kwa ujumla wanashauriwa kuendelea kufuatilia na kuzingatiabtaarifa za utabiri kutoka Mamlaka ya hali ya hewa nchini pamoja na kupata ushauri na miongozo ya wataalam wa kisekta,”imesema
Aidha TMA inaendelea kufuatilia mwenendo wa kimbunga hicho na athari zake kwa mifumo ya hali ya hewa hapa nchini na itaendelea kutoa taarifa kila inapobidi.
More Stories
Simbachawene:Mfumo wa Tathmini ya Mahitaji Rasilimaliwatu umebaini upungufu wa watumishi 441,366
Wakazi Arusha watakiwa kuchangamkia fursa huduma jumuishi za kifedha
Wahitimu wa Mafunzo ya Scout Nkasi watakiwa kuwa mwangaza kwa vijana