Na Heri Shaaban, Timesmajira Online
MAMLAKA ya Hali ya Hewa Tanzania(TMA) imesema hali ya hewa kwa saa 24 zijazo baadhi ya mikoa inatazamiwa kuwa na vipindi vya upepo mkali.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na TMA vipindi vya upepo mkali vinatazamiwa katika maeneo ya mikoa ya Pwani ya Bahari ya Hindi,Lindi,Mtwara, Tanga,Dar es Salaam ikijumuisha Visiwa vya Mafia,Unguja na Pemba .
Aidha kwa mujibu wa TMA tahadhari nyingine ya vipindi vya upepo mkali imetolea kwa mikoa ya Ukanda wa Ziwa Nyasa ,Mikoa ya Njombe ,Ruvuma na Mbeya pamoja na mikoa ya Ukanda wa Kusini mwa mikoa ya ziwa Tanganyika, Mikoa ya Katavi na Rukwa.

More Stories
Waziri Kikwete akutana na viongozi Chalinze wajadili Dira 2050
Kampuni ya Oryx Gas yakabidhi mitumgi 600 kwa wajasiriamali
DCEA yafanikiwa kuteketeza ekari 291.2 Mara