Na Joyce Kasiki,Dodoma
MAMLAKA ya Bima Tanzania imewaasa wananchi wajifunze na watumie bidhaa za Bima za kilimo,ufugaji na uvuvi ili waweze kujilinda dhidi ya majanga.
Hatua hiyo itamwezesha mkulima,mfugaji na mvuvi kulinda uwekezaji wao kwa kufidiwa pindi yanapotokea majanga.
Kamishna wa Bima Tanzania Dkt.Baghayo Saqware ameyasema hayo wakati akizungumza na waandishi wa habari kwenye kilele cha cha maadhimisho ya siku kuu ya wakulima,wafugaji na wavuvi (Nane nane ) katika viwanja vya Nzuguni jijini Dodoma.
“Bidhaa za bima husaidia muhusika kufidiwa pindi yanapotokea majanga yatokanayo na mafuriko,wadudu waharibifu,ukame ,majanga ya moto kwenye mashamba na kuharibu mazao ,yote hayo yanalipwa na kampuni za Bima.” Amesema
Ameongeza kuwa “Kwa hiyo tunawasihi wakulima ,wafugaji na wavuvi waje wakate bima .”amesema Saqware
Dkt.Saqware amesema kuwa katika sekta hizo watu wamekuwa wakitumia fedha nyingi kufanya uwekezaji huku akisema uwekezaji huo unatakiwa ulindwe kwa bima.
“Ukikata Bima uwekezaji wako wote uliowekeza kwa fedha nyingi unalindwa kwa gharama kidogo na bima ,
More Stories
Kamati ya kudumu ya Bunge ya utawala,katiba na sheria yaridhishwa ujenzi soko Kariakoo
TRA Tanga yakusanya bil.178.3 kwa miezi sita
Wataalam Sekta ya utalii watakiwa kufanya kazi kwa uadilifu,kujituma na kuwa wabunifu