Na Mwandishi wetu, TimesMajira Online
Tigo wameshinda Tuzo ya Usalama na Afya Mahali pa kazi inayotolewa na Wakala wa Usalama na Afya Mahali (OSHA) Jijini Dodoma. Tuzo imekabidhiwa na Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi, Ajira, Vijana na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako.
Tigo wanatambua umuhimu wa usalama na afya mahali pa kazi mara zote. Hivyo basi wamefanya tathimini ya usalama wa wafanyakazi wetu mahali kwa kazi ili kuendelea kutoa huduma na bidhaa bora kwa wateja wao mara zote.

Pia Tigo wamesema watahakikisha, wanaelimisha na kuhamasisha masuala ya Usalama na Afya Mahali pa kazi pamoja kwa kuweka mifumo thabiti itakayo zuia ajali kwa kuchukua tahadhali mapema, magonjwa na vifo pamoja na uharibifu wa mali ikiwa lengo ni kupunguza gharama za uendeshaji nk

Kauli Mbiu ya Mwaka 2022: Act Together to build Healt and Safety Culture.
More Stories
YAS yatoa Elimu ya mtandao Karibu Kill Fair ,yajipanga kuinua sekta ya utalii
Puma Energy Yazindua Mradi wa Umeme wa Jua kwa Kiwanda cha Alliance One
Exim yatangaza mafanikio makubwa na mwelekeo madhubuti 2025