Na Mwandishi wetu, Timesmajira
Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) limeanza utekelezaji wa mpango kabambe wa kuimarisha njia za kusambazia umeme na kuongeza ubora wa Nishati ya Umeme katika maeneo mbalimbali ya Mkoa wa kiTANESCO wa Kigamboni.
Mpango huu uliopewa jina la Umeme Bora Kigamboni umekuja baada ya maeneo ya baadhi ya maeneo ya Kigamboni kukumbwa na adha ya kukatika katika kwa umeme kulikosababishwa na ongezeko kubwa la mahitaji ya umeme pamoja na uchakavu wa miundombinu unaoathiri ufanisi wa utoaji wa huduma katika maeneo hayo.

Mpango huu unalenga kutekeleza Miradi 35 ya kuboresha ubora wa nguvu za umeme yaani (Voltage Improvement Project) na unatarajiwa kukamilishwa sambamba na matengenezo makubwa kwenye njia 8 (Feeders) za kusambazia umeme.
Akizungumza katika moja ya maeneo ambayo TANESCO wanatekeleza Mradi Mwenyekiti wa Serikali ya mtaa wa Kifurukwe,Sultan Mbebe ameishukuru Serikali kupitia TANESCO kwa kuanza utekelezaji wa miradi hiyo.
More Stories
Chalamila:Dar ni salama,aelezea mafanikio na mipango ya maendeleo ya Mkoa
Ulaji vyakula vya aina moja,umri vyatajwa ongozeko la matatizo ya macho Mbeya
Kenya,Uganda zaanzisha mradi wa uendelezaji rasilimali za maji Angololo