Na James Mwanamyoto,TimesMajira Online. Dodoma
MAOFISA Utumishi watakaozembea na kusababisha watumishi wa umma kutolipwa mishahara yao kwa wakati, watasimamishiwa mishahara na serikali mpaka watakapohakikisha watumishi hao wamelipwa mishahara yao.
Hayo yamesemwa jana na Kaimu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Dkt. Francis Michael wakati akifungua mafunzo ya wiki mbili ya Mfumo Mpya wa Kitanzania wa Taarifa za Kiutumishi na Mishahara kwa kundi la pili la Maofisa Utumishi na Maofisa Tawala 140 kutoka Mikoa ya Mwanza, Shinyanga, Mara, Manyara, Arusha, Kilimanjaro, Tanga, Pwani, Dar es Salaam, Lindi, Mtwara, Kigoma na Tabora yanayofanyika jijini Dodoma katika Ukumbi wa VETA.
DKt. Michael amesema, kuna tatizo katika baadhi ya taasisi za umma kwani wapo Maofisa Utumishi wanajifanya miungu watu, wakati wajibu wao ni kumtengenezea mazingira mazuri ya kikazi mtumishi ili ajisikie yuko sehemu salama na aweze kutekeleza ipasavyo jukumu la kuwahudumia wananchi.
“Msiwafanye watumishi mnaowasimamia kuona sehemu ya kazi kama jehanamu, hivyo mbadilike kwani serikali haitomvumilia yeyote atakayekinzana na azma yake ya kuboresha huduma kwa wananchi,” amesema.
More Stories
Rais Samia amrudisha January kwa Mama,asema kilichotokea ni kumuonya
Milioni 236 kunufaisha vikundi 17 vya wanawake Minazi Mirefu
Mipango 10 kabambe ya TPA