Na Joyce Kasiki,Timesmajira online,Dodoma
SERIKALI inatarajia kuzindua Sera ya Ardhi ya Mwaka 1995 ,Toleo la 2023 iliyolenga kuongeza ufanisi katika sekta ya ardhi kwa ujumla
Akizungumza Machi 15 mwaka huu na waandishi wa habari Jijini Dodoma,Waziri wa Ardhi,Nyumba na Maendeleo ya Makazi Deogratius Ndejembi amesema uzinduzi huo utafanyika Machi 17 mwaka huu katika ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete.
“Sera hii inalenga kuimarisha usimamizi wa ardhi kwa kuongeza ufanisi wa utawala, kutatua migogoro ya ardhi, na kuweka mifumo inayosomana ili kurahisisha upatikanaji wa taarifa na ufuatiliaji wa shughuli za ardhi.”alisema Ndejembi na kuongeza kuwa
“Sera hii itaongeza uwazi na ushirikishwaji wa wananchi katika masuala ya ardhi, kuwezesha uwekezaji endelevu, na kulinda haki za wamiliki wa ardhi vijijini na mijini.”
Ndejembi alisema,uzinduzi huo utahudhuriwa na wageni mbalimbali wakiwemo mabalozi wanaowakilisha Nchi zao hapa nchini pamoja na Wadau wa ardhi
Aidha alisema Sera hiyo itazinduliwa na Rais Dkt Samia Suluhu Hassan huku akisema kaulimbiu ya uzinduzi huo ni “Sera ya Ardhi Msingi wa Ustawi na Malengo Endelevu ya Taifa”
More Stories
Hospitali ya Rufaa Kanda ya Mbeya kuanzisha matibabu ya upasuaji moyo
VETA wapaka rangi jengo la watoto MNH ,wakisherekea miaka 30
Waziri Silaa ashiriki kupandisha vifaa ujenzi wa Mnara wa mawasiliano Idete