Na Mwandishi Wetu,Timesmajira
RAIS Samia Suluhu Hasan, anatarajia kuhudhuria Mkutano wa 44 wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) utakaofanyika Agosti 17, 2024 mjini Harare, Zimbabwe.
Rais Dkt. Samia anaondoka nchini leo Agosti 15, 2024
kuhudhuria Mkutano huo wenye kauli mbinu: “Kukuza ubunifu ili kufungua
fursa za ukuaji wa uchumi na maendeleo endelevu kuelekea SADC yenye
viwanda.”
Katika Mkutano huo, Rais Dkt. Samia anatarajia kuchaguliwa kuwa
Mwenyekiti wa Asasi ya Siasa, Ulinzi na Usalama ya SADC akipokea kutoka
kwa Rais wa Jamhuri ya Zambia Hakainde Hichilema anayemaliza muda
wake.

More Stories
Serikali yaagiza usalama migodini Lindi
Awamu ya kwanza ya uvutaji wa nyaya katika Mradi wa Chalinze -Dodoma wakamilika
EWURA yatangaza bei ya mafuta