May 3, 2024

Timesmajira

Gazeti Huru La Kila Siku

Rais Samia azindua Jengo la Makao Makuu ya Benki ya CRDB

Na Mwandishi wetu, TimesMajira Online

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan akiwa na Mkurugenzi Mtendaji wa CRDB Abdulmajid Nsekela pamoja na viongozi wengine Wakuu wa CRDB pamoja na Serikali akivuta kitambaa kuashiria ufunguzi wa Jengo la Makao Makuu ya Benki hiyo yaliyopo Palm Beach, Mkabala na Barabara ya Ali Hassan Mwinyi Jijini Dar es Salaam leo tarehe 05 March 2022.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan akiwa na viongozi wengine Wakuu wa CRDB pamoja na Serikali akiminya kitufe kuashiria ufunguzi wa Jengo la Makao Makuu ya Benki ya CRDB lililopo Palm Beach, Mkabala na Barabara ya Ali Hassan Mwinyi Jijini Dar es Salaam.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu akiwa pamoja na Wajumbe wa Bodi ya Benki ya CRDB pamoja na viongozi wengine wa Serikali katika ukumbi wa Mikutano wa Makao Makuu ya Benki ya CRDB yaliyopo pembezoni mwa Barabara ya Ali Hassan Mwinyi Jijini Dar es Salaam.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu akizungumza na viongozi mbalimbali pamoja na Wafanyakazi wa CRDB mara baada ya kuzindua jengo la Makao Makuu ya Benki ya CRDB yaliyopo pembezoni mwa Barabara ya Ali Hassan Mwinyi Jijini Dar es Salaam.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu akiagana na viongozi mbalimbali wa Benki ya CRDB mara baada ya kuzungumza nao katika viwanja vya Agha Khan Jijini Dar es Salaam.