Na Penina Malundo, TimesMajira Online
Rais Samia Suluhu Hassan ametimiza ahadi ya kumpatia mtaji wa Biashara na fedha za kujikimu Yassin Said mwenye Ulemavu wa Ngozi ambaye aliemuandikia barua Rais Samia akiomba kuwezeshwa kiuchumi baada ya kupitia masaibu katika maisha yake.
Akikabidhi fedha hizo kwa niaba ya *Rais Samia, Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Amos Makalla amemsisitiza Kijana huyo kutumia fedha alizopatiwa kujiimarisha kiuchumi ili lengo la Rais Samia kutoa fedha hizo liweze kutimia.
Kwa upande wake Said amemshukuru Rais Samia kwa msaada aliopatiwa na kuahidi kuzitumia fedha hizo kwa lengo lililokusudiwa.
More Stories
Yas yaja na ‘Anzia Ulipo’ kuhamasisha watanzania kusimamia ndoto zao
Coca-Cola Kwanza kuwanufaisha mama lishe Stendi ya Msamvu Marogoro
Sheikh Ponda akabidhiwa kadi ya heshima ya Maalim Seif