Na Penina Malundo, TimesMajira Online
Rais Samia Suluhu Hassan ametimiza ahadi ya kumpatia mtaji wa Biashara na fedha za kujikimu Yassin Said mwenye Ulemavu wa Ngozi ambaye aliemuandikia barua Rais Samia akiomba kuwezeshwa kiuchumi baada ya kupitia masaibu katika maisha yake.
Akikabidhi fedha hizo kwa niaba ya *Rais Samia, Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Amos Makalla amemsisitiza Kijana huyo kutumia fedha alizopatiwa kujiimarisha kiuchumi ili lengo la Rais Samia kutoa fedha hizo liweze kutimia.
Kwa upande wake Said amemshukuru Rais Samia kwa msaada aliopatiwa na kuahidi kuzitumia fedha hizo kwa lengo lililokusudiwa.
More Stories
Bilioni 15 kukopeshwa wanawake,vijana jijini Dar
Serikali yaendelea kubuni mbinu kukabiliana na wanyamapori wakali
Wanaodaiwa kufukua kaburi na kuondoka na mwili wa marehemu watafutwa