Na Mwandishi Wetu, TimesMajira Online
RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan leo tarehe 19 Juni, 2021 amefanya uteuzi wa Wenyeviti wanne (4) wa Bodi za Wakurugenzi kama ifuatavyo:-
- Amemteua Dkt. Fenella Ephraim Mukangara kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Shirika la Viwango Tanzania (TBS). Dkt. Mukangara ni Mhadhiri Mwandamizi Mstaafu Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM).
- Amemteua Brig. ( Mstaafu) Aloyce Damian Mwanjile kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Korosho Tanzania.
- Amemteua Bw. Khalfan Ramadhani Khalfan kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC).
- Amemteua Capt. Mussa Mandia kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania (TASAC).
Uteuzi huo unaanza leo tarehe 19 Juni, 2021.
More Stories
Mke wa Rais wa Msumbiji,Gueta atembelea JKCI
Kadinali Robert Prevost achaguliwa kuwa Papa Leo wa XIV
Viongozi wa Dini waaswa kuimarisha mafundisho kwa wanandoa kunusuru kuvunjika kwa ndoa