Na Mwandishi Wetu, TimesMajira Online
RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan leo tarehe 19 Juni, 2021 amefanya uteuzi wa Wenyeviti wanne (4) wa Bodi za Wakurugenzi kama ifuatavyo:-
- Amemteua Dkt. Fenella Ephraim Mukangara kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Shirika la Viwango Tanzania (TBS). Dkt. Mukangara ni Mhadhiri Mwandamizi Mstaafu Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM).
- Amemteua Brig. ( Mstaafu) Aloyce Damian Mwanjile kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Korosho Tanzania.
- Amemteua Bw. Khalfan Ramadhani Khalfan kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC).
- Amemteua Capt. Mussa Mandia kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania (TASAC).
Uteuzi huo unaanza leo tarehe 19 Juni, 2021.

More Stories
Bilioni 7 kuwainua vijana 308 sekta ya uvuvi
Clara:Miaka 50 ya Sabasaba fursa mpya za Biashara na Uwekezaji
Usajili wa Laini za Simu: Jilinde Dhidi ya Kutumiwa Vibaya kwa Utambulisho Wako