March 7, 2026

Timesmajira

Gazeti Huru La Kila Siku

Rais Samia atangaza Baraza jipya la Mawaziri, Aweso, Kundo warejea Wizara ya Maji

Na Mwandishi Wetu, Timesmajira Online 

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan ametangaza Baraza la Mawaziri,huku akimteua Jumaa  Aweso na Mhandisi Kundo Mathew kwa mara nyingine kuongoza Wizara ya Maji.

Akitangaza baraza hilo  Novemba 17,2025  Ikulu ya Chamwino, Dodoma, Rais Dkt.Samia ameunda Wizara 27 na kuteua  Mawaziri  27 na Manaibu Mawaziri 29, ambapo amemteua  kwa mara nyingine Jumaa Aweso kushika nafasi ya  Waziri wa Maji huku Mhandisi Mathew Kundo kushika nafasi  Naibu Waziri wa Wizara  hiyo.

Pia  Dkt.Samia amewateu kwa mara nyingine  Abdallah Ulega kuwa Waziri  wa Ujenzi  na  Mhandisi Godfrey Kasekenya kuwa Naibu Waziri wa Wizara hiyo pamoja na Profesa Kitila Mkumbo kuendelea  kuwa Waziri wa Ofisi ya Rais – Mipango na Uwekezaji.

Mwingine ni Dkt.Doroth Gwajima ambaye ameteuliwa kwa mara nyingine kuwa Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum,huku katika Wizara ya Uchukuzi Prof. Makame Mbarawa akiendelea kuongoza Wizara hiyo kwa mara nyingine.

Sanjari na hayo Dkt.Samia katika  Wizara ya Ofisi ya Rais – Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora amemteua Ridhiwani Kikwete  kuwa Waziri huku Naibu Waziri ni Regina Qwaray.

Ofisi ya Rais -Maendeleo ya Vijana

Waziri ni Joel Nanauka huku Ofisi ya Makamu wa Rais – Muungano na Mazingira Waziri ni  Mhandisi Hamad Masauni na  Naibu Waziri ni Dkt. Festo Dugange

Hata hivyo Ofisi ya Waziri Mkuu – Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu ni  Waziri  William Lukuvi huku Naibu Waziri: ni Ummy  Nderiananga.