Na Mwandishi Wetu,Timesmajiraonline, Moro
RAIS Samia Suluhu Hassan ameiagiza Wizara ya Nishati kuongeza nguvu katika kusimamia miradi yote ya nishati ili ikamilike kwa wakati na hivyo kuwawezesha wananchi kupata nishati ya uhakika.
Rais Samia alitoa agizo hilo juzi, Agosti 06, 2024 wakati akihitimisha ziara yake ya kikazi mkoani Morogoro.
“Nimejionea mwenyewe wakati naenda Kilosa tofauti iliyokuwa ikionekana maeneo ambayo hayana umeme na yale yenye umeme ambayo yameshamiri kwa shughuli za biashara, hii inaonesha umuhimu wa nishati katika maeneo yote nchini.” Alisisitiza Dkt.Samia
Aidha, Rais Samia aliutaka Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kukamilisha mapema kupeleka umeme kwenye Vijiji vilivyobaki na kuongeza kasi ya kusambaza umeme kwenye Vitongoji ili wananchi waweze kufanya kazi za maendeleo.
Aidha, alisisitiza kuwa uwepo wa umeme wa uhakika kutoka Bwawa la Julius Nyerere kunaufanya Mkoa wa Morogoro kuwa sehemu sahihi ya uwekezaji.
“Morogoro sasa ina umeme wa uhakika, hali inayovuta uwekezaji ndani ya Mkoa.” Aliongeza Rais
Akizungumzia kuhusu miradi ya umeme vijijini Mkoa wa Morogoro, Dkt. Samia amesema kupitia Wakala wa Nishati Vijijini Serikali imepeleka umeme kwenye Vijiji 621 kati ya Vijiji 669.
More Stories
Mjumbe UWT Taifa awataka vijana kutokubali kutumika kuvuruga amani
Dkt.Mabula aomba mabonde Ilemela yatumike kwa Kilimo cha umwagiliaji
Ubovu wa barabara mlima Kilimanjaro, changamoto watalii kufikia vivutio vya utalii