Na Mwandishi wetu, TimesMajira Online
Rais wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan amegiza Vyombo vya Uchunguzi kumpatia taarifa ya kina haraka kuhusu tukio baya la mauaji ya Kiongozi wa CHADEMA Ali Kibao na mengine ya namna hiyo.
Rais Samia amesema “Nchi yetu ni ya kidemokrasia na kila raia ana haki ya kuishi, Serikali ninayoiongoza haivumilii vitendo vya kikatili vya namna hii”
“Kwa masikitiko makubwa nimepokea taarifa ya mauaji ya kiongozi wa CHADEMA Bwana Mohamed Ali Kibao, natoa pole kwa Viongozi wa Chama hicho, Familia ya Mzee Kibao, Ndugu, Jamaa na Marafiki.


More Stories
Tanzania mwenyeji wa mkutano wa Wanahisa wa Africa50, Jukwaa la miundombinu Afrika
Yas yazindua Mnara wa 5G Masasi
Wafanyabiashara wahimizwa kutumia nembo ya Tanzania