June 3, 2025

Timesmajira

Gazeti Huru La Kila Siku

Rais Samia apongezwa kuwezesha mkutano wa IGF

Na Heri Shaaban,Timesmajiraonline,Dar

Mratibu wa Jukwaa la Usimamizi wa Unternal Tanzania (IGF)Dkt.Nazar Kirama amempongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.Samia Suluhu Hassan kwa kuwezesha mkutano wa mtandao nchi za Afrika wa masuala ya intaneti kufanyika Tanzania.

Dkt. Kirama ,amesema hayo jijini hapa Mei 31,2025  katika mkutano wa 14 wa nchi za Afrika kuhusiana na masuala ya intaneti katika ukumbi wa mwalimu Nyerere.

“Jukwaa la usimamizi wa Unternal Tanzania tunampongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.Samia Suluhu  nchi yetu kupewa heshima  katika mkutano wa masuala ya intaneti kwa nchi za Afrika “amesema Dkt.Kirama.

Dkt.Kirama amesema kufanyika kwa mkutano huo hapa nchini unatokana na mkutano wa awali uliofanyika nchini Uswizi.

Amesema kulikuwa  na majadiliano mazuri awali katika  mkutano wa wabunge wa Afrika kutoka jukwaa hilo ambalo linajumuisha wadau mbalimbali wanaoshiriki katika sera za nchi moja moja na kuleta mafanikio  .

Aidha amesema kupitia mkutano huo utakuza sekta ya uchumi katika masuala ya intaneti na mfumo wa TEHAMA  ambapo vijana wakitumia vizuri kupitia simu janja na YouTube chanel wataweza kupata kipato ajira na kuongezeka.